Dominiko Savio

From Wikipedia, the free encyclopedia

Dominiko Savio
Remove ads

Dominiko Savio (Kiitalia: Domenico Savio; Riva presso Chieri, 2 Aprili 1842Castelnuovo Don Bosco, 9 Machi 1857[1][2]) alikuwa mvulana wa Italia aliyelelewa na Yohane Bosco kufuata upole na furaha na kwa njia hiyo alifikia mapema ukamilifu wa Kikristo [3].

Thumb
Mt. Dominic Savio.

Akiwa anasomea upadri aliugua na hatimaye akafariki dunia katika umri wa miaka 14 tu.[4]

Mlezi wake aliandika kitabu juu yake (Maisha ya Dominiko Savio) ambacho kilichangia sana kumfanya ajulikane na hatimaye atangazwe na Papa Pius XII kwanza mwenye heri tarehe 5 Machi 1950, halafu mtakatifu[5] tarehe 12 Juni 1954.[6]

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyofariki dunia[7].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads