Engrasya

From Wikipedia, the free encyclopedia

Engrasya
Remove ads

Engrasya (Braga, Ureno, karne ya 3 - Zaragoza, Hispania, 304 hivi) alikuwa bikira aliyestahimili mateso na kifodini katika dhuluma ya kaisari Dioklesyano dhidi ya Wakristo [1]. Siku hizi wengine wanamtaja kaisari Valerian (254-260)[2]

Thumb
Mt. Engrasya alivyochorwa.

Heshima ya watu kwake kama mtakatifu ni ya zamani sana. Mshairi Prudentius (348-410), mwenyeji wa mji huo, alitunga utenzi juu yake na ya wafiadini wenzake[3].

Sikukuu yake huadhimishwa kila mwaka tarehe 16 Aprili[4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads