Visiwa vya Falkland

From Wikipedia, the free encyclopedia

Visiwa vya Falkland
Remove ads

Visiwa vya Falkland (kwa Kiingereza: Falkland Islands; kwa Kihispania Islas Malvinas) ni funguvisiwa katika bahari ya Atlantiki ya kusini takriban km 450 mbele ya pwani ya Argentina.

Ukweli wa haraka


Thumb
Kanisa kuu la Christchurch, Stanley.
Thumb
Nyumba ya mkulima katika nyika za Falkland.

Falkland ni eneo la ng'ambo la Uingereza linalodaiwa na Argentina kama sehemu yake. Hivyo mwaka 1982 jeshi la Argentina ilivamia visiwa vikuu. Uingereza ilijibu kivita ikapeleka wanajeshi huko na baada ya vita vifupi vya wiki 6 Argentina ilishindwa; takriban wanajeshi 1,000 waliuawa.

Remove ads

Jiografia

Funguvisiwa lina takriban visiwa 200. Viwili ambavyo ni vikubwa ni Falkland Magharibi na Falkland Mashariki na kila kimoja huwa na eneo la takriban km² 6,000. Mwinuko mkubwa ni mlima Usborne (Kihispania: Cerro Alberdi) wenye kimo cha mita 708 juu ya uwiano wa bahari.

Hali ya hewa ni baridi na kuna mvua nyingi. Halijoto ya wastani ni 5 °C pekee. Kwa sababu hiyo mimea ni hasa nyasi; kutokana na baridi miti haizidi kimo cha mita 1.

Remove ads

Watu

Idadi ya wakazi imepita 3,000 na wote hao ni Waingereza wanaosema Kiingereza. Wanajipatia riziki zao kwa uvuvi na ufugaji wa kondoo.

Upande wa dini, 66% ni Wakristo, hasa Waanglikana, lakini pia Wakatoliki na wengineo. 32% hawana dini yoyote.

Mji pekee ambao ni pia makao makuu ya utawala ni Port Stanley kwenye kisiwa cha mashariki wenye wakazi 2,100. Pamoja na wakazi kuna wanajeshi Waingereza 1,500.

Barabara ya lami ya pekee kisiwani ni ile inayounganisha Stanley na kituo cha kijeshi kwa umbali wa kilomita 50.

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads