Guadeloupe

département ya Ufaransa From Wikipedia, the free encyclopedia

Guadeloupe
Remove ads

Guadeloupe ni eneo la ng'ambo na mkoa (departement) wa Ufaransa katika Bahari ya Karibi lenye visiwa tisa vidogo. Hivyo ni sehemu ya Umoja wa Ulaya.

Thumb
Guadeloupe,Ufaransa
Ukweli wa haraka Nchi, Mji mkuu ...
Remove ads
Thumb
Maeneo mweupe ni sehemu za Guadeloupe

Makao makuu ni Basse-Terre, ingawa mji mkubwa ni Pointe-à-Pitre.

Wakazi asilia walikuwa Waindio. Utamaduni wao uliharibiwa kabisa kwa kuja kwa ukoloni kutoka Ulaya (1493).

Ilikuwa koloni la Ufaransa halafu la Uingereza halafu la Uswidi halafu la Ufaransa tena.

Eneo lake ni km² 1,628.

Remove ads

Watu

Idadi ya wakazi ni 394,110. Asilimia 71 za wakazi ni wa asili ya Afrika au machotara. Wazee wao waliletwa huko kama watumwa kwa ajili ya kazi za mashamba ya miwa. 15% ni Wahindi, 9% Wazungu, 3% Wachina na 2% Waarabu.

Lugha rasmi ni Kifaransa, lakini wengi wanaongea pia Krioli.

Upande wa dini, 80% ni Wakatoliki na 5% Waprotestanti.

Tazama pia

  • Martinique, eneo lingine la Ufaransa katika Bahari ya Karibi

Viungo vya nje

Serikali

Safari

Makala hii kuhusu maeneo ya Bahari ya Karibi bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Guadeloupe kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Remove ads
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads