Habakuki

From Wikipedia, the free encyclopedia

Habakuki
Remove ads

Habakuki alikuwa nabii wa Israeli ya Kale aliyeishi na kufanya kazi wakati mmoja na nabii Yeremia (karne ya 7 KK).

Thumb
Sanamu ya Habakuki iliyotengenezwa na Donatello, Museo dell'Opera del Duomo, Florence.

Mbele ya uovu na ukatili wa binadamu alitabiri hukumu ya Mungu, lakini pia huruma yake[1].

Hababuki aliandika kitabu kifupi ambamo alithubutu kumuuliza Mwenyezi Mungu kwa nini anaadhibu Israeli vikali kwa mikono ya watu wabaya kuliko wao.

Jibu ni kwamba Mwenyezi Mungu ana njia zake ambazo anaandaa ushindi wa haki: hivyo mwadilifu ataishi kwa imani yake (1:12-2:4).

Usemi huo ukaja kutumika sana katika Agano Jipya. Mtume Paulo ameufanya msingi wa msimamo wake kuwa wokovu unapatikana kwa imani, si kwa kujitahidi kutekeleza masharti yote ya Torati.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 2 Desemba[2][3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads