Isaka Mkuu

From Wikipedia, the free encyclopedia

Isaka Mkuu
Remove ads

Isaka Mkuu (pia: Sahak Partev; 354 hivi - Bagrevand, 439) alikuwa mmonaki, mwanateolojia na askofu kutoka Armenia ya Kale.

Thumb
Mt. Isaka Mkuu alivyochorwa.

Mtoto wa Nerses I na kilembwekeza wa Gregori Mletamwanga, alipofiwa mke wake alijiunga na monasteri, halafu kama Patriarki alipigania umoja wa Kanisa kwa msingi wa imani sahihi ya Mtaguso wa Efeso, lakini akaja kufukuzwa jimboni akafariki uhamishoni.

Pia alisaidiana na Mesrop kutafsiri Biblia na alirekebisha liturujia na sheria za Kanisa[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Septemba[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads