Malaika Gabrieli

From Wikipedia, the free encyclopedia

Malaika Gabrieli
Remove ads
Remove ads

Malaika Gabrieli (kwa Kiebrania גַּבְרִיאֵל, Gavri'el, Gaḇrîʼēl, Mungu ni nguvu yangu; kwa Kiarabu جبريل, Jibrīl au جبرائيل Jibrāʾīl) ni malaika aliyetumwa na Mungu kuleta ujumbe wa pekee[1] katika dini zinazotaka kufuata imani ya Abrahamu.

Thumb
Picha ya Gabrieli kwa mtindo wa Kiorthodoksi, 13871395 hivi (Tretyakov Gallery).
Thumb
Mchoro wa Bikira Maria kupashwa habari na Gabrieli, kazi ya Anton Raphael Mengs.

Kwa sababu hiyo Wakatoliki, kuanzia Pseudodionisi na Papa Gregori I, wanamheshimu kama malaika mkuu pamoja na malaika Mikaeli na malaika Rafaeli, hasa tarehe 29 Septemba[2][3].

Wakristo wengine pia wanamheshimu kwa kupasha habari ya kutungwa mimba kwa Yohane Mbatizaji[4], halafu kwa Yesu[5] inavyosimuliwa na Injili ya Luka.

Waislamu pia wanamheshimu kwa ajili hiyo na kwa kumletea Mtume Muhammad ufunuo wa Kurani.

Kwa mara ya kwanza jina lake liliandikwa katika kitabu cha Danieli (8:15-26; 9:21-27).

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading content...

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Loading content...

Viungo vya nje

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads