Kanuti IV

From Wikipedia, the free encyclopedia

Kanuti IV
Remove ads

Kanuti IV (maarufu kwa Kidani kama "Knud den Hellige", yaani "Kanuti mtakatifu", 1043 - Odense, 10 Julai 1086), alikuwa mfalme wa Udani kuanzia mwaka 1080 hadi siku ya kuuawa.

Thumb
Uuaji wa Mt. Kanuti ulivyochorwa na Christian Albrecht von Benzon, 1843.

Pamoja na utakatifu wake, alionyesha bidii kubwa kwa ajili ya ibada na mahitaji ya wakleri pamoja na uimarishaji wa mamlaka yake ndani na nje ya nchi[1].

Baada ya kuanzisha makanisa ya Lund na Odense, aliuawa ndani ya hilo, mbele ya altare, pamoja na watu wengine 8 au 18.

Wananchi walimheshimu mara moja kama mtakatifu, na Papa Paskali II alithibitisha heshima hiyo mwaka 1101.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifodini chake[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads