Klod

From Wikipedia, the free encyclopedia

Klod
Remove ads

Klod (kwa Kifaransa Cloud; kwa Kilatini Clodoaldus; 522 - 560 hivi) alikuwa padri kutoka ukoo wa kifalme wa Orleans huko Ufaransa [1].

Thumb
Sanamu ya Mt. Klod.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Septemba[2].

Maisha

Babu yake alikuwa Klovis I na bibi yake alikuwa mtakatifu Klotilda malkia.

Baba yake, mfalme Klodomer[3], na ndugu zake wawili waliuawa wakiwa bado watoto; yeye tu alinusurika kwa kumkimbilia bibi yake huko Provence[4] na kujinyima haki zote za kurithi. Pia aliwagawia fukara mali iliyombakia.

Baada ya kuishi kama mkaapweke chini ya Severini wa Paris, alipoona anatembelewa na watu wengi kwa ushauri kiasi kwamba hafaidiki na upweke akarudi Paris, alipopokewa kwa furaha.

Watu walimuomba askofu ampe upadrisho (551). Halafu alitoa huduma kwa muda fulani, kisha akarudi upwekeni, na hatimaye akaanzisha abasia karibu na Versailles[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads