Klod
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Klod (kwa Kifaransa Cloud; kwa Kilatini Clodoaldus; 522 - 560 hivi) alikuwa padri kutoka ukoo wa kifalme wa Orleans huko Ufaransa [1].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 7 Septemba[2].
Maisha
Babu yake alikuwa Klovis I na bibi yake alikuwa mtakatifu Klotilda malkia.
Baba yake, mfalme Klodomer[3], na ndugu zake wawili waliuawa wakiwa bado watoto; yeye tu alinusurika kwa kumkimbilia bibi yake huko Provence[4] na kujinyima haki zote za kurithi. Pia aliwagawia fukara mali iliyombakia.
Baada ya kuishi kama mkaapweke chini ya Severini wa Paris, alipoona anatembelewa na watu wengi kwa ushauri kiasi kwamba hafaidiki na upweke akarudi Paris, alipopokewa kwa furaha.
Watu walimuomba askofu ampe upadrisho (551). Halafu alitoa huduma kwa muda fulani, kisha akarudi upwekeni, na hatimaye akaanzisha abasia karibu na Versailles[5].
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo ya Kiswahili
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads