Maruta

From Wikipedia, the free encyclopedia

Maruta
Remove ads

Maruta (karne ya 4415) alikuwa mmonaki wa Kanisa la Mashariki[1] maarufu kama askofu wa Mayferkat (leo Silvan nchini Uturuki) kwa zaidi ya miaka 10 ambapo alifaulu kuzuia dhuluma ya Dola la Persia dhidi ya Wakristo[2].

Thumb
Mchoro mdogo ukimwonyesha Mt. Maruta askofu.

Hivyo aliweza kujenga upya makanisa, kukusanya humo masalia ya wafiadini, kuendesha sinodi mbili zilizolipa Kanisa hilo muundo imara, pamoja na kuandika vitabu vya historia ya Kanisa na ufafanuzi wa Biblia, tenzi, anafora n.k.[3]

Rafiki wa Yohane Krisostomo, alishiriki Mtaguso wa kwanza wa Konstantinopoli (481)[4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 16 Februari[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads