Mbamba Bay

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Mbamba Bay ni kata na makao makuu ya Wilaya ya Nyasa katika Mkoa wa Ruvuma, Tanzania.

Ukweli wa haraka Nchi, Mkoa ...

Jina

Maana ya Mbamba Bay ni neno Mbamba ambalo ni jina la mlima uliopo eneo la Zambia na Bay, kama inavyojulikana, ni eneo la bahari lililoingia ndani kama Oyster Bay, Mnazi Bay n.k.

Wakazi

Katika sensa iliyofanyika mwaka 2022 wakazi walihesabika kuwa 13,463 [1]. Kwa mujibu wa sensa iliyofanyika mwaka 2012, kata ya Mbamba Bay ilikuwa na wakazi wapatao 10,066 waishio humo. [2]

Thumb
Mbamba Bay ufukoni mwa Ziwa Nyasa.
Thumb
Picha ya Mbamba Bay kabla ya mwaka 1900.

Jiografia

Mji wa Mbamba Bay uko kwenye ufuko wa Ziwa Nyasa takriban km 20 upande wa kaskazini wa mpaka kati ya Tanzania na Msumbiji.

Usafiri

Kuna bandari inayohudumiwa na meli SV Songea. Kwa ratiba isiyofuatwa mara kwa mara kuna mawasiliano pia na Nkhata Bay huko Malawi, ng'ambo ya ziwa, halafu kwa bandari nyingine za mwambao wa Kitanzania za Ziwa Nyasa hadi Itungi Port.

Kulikuwa na majadiliano ya kujenga reli Mbamba Bay - Mtwara kwa ajili ya usafiri mfupi kati ya Malawi na Bahari Hindi na pia kwa kuboresha maendeleo kusini mwa Tanzania (Mtwara Development Corridor).

Remove ads

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads