Mkoa wa Ruvuma

From Wikipedia, the free encyclopedia

Mkoa wa Ruvuma
Remove ads

Mkoa wa Ruvuma ni kati ya mikoa 31 ya Tanzania. Umepewa jina kutokana na mto Ruvuma ambao ni mpaka wake wa kusini na Msumbiji. Pia unapakana na Ziwa Nyasa na Mkoa wa Morogoro upande wa magharibi, mikoa ya Njombe na Lindi upande wa kaskazini na Mkoa wa Mtwara upande wa mashariki. Eneo lote ni la km2 63,669. Jumla ya wakazi wote katika Mkoa wa Ruvuma ni 1,848,794 (sensa ya mwaka 2022). Makao makuu ya mkoa yako Songea mjini.

Ukweli wa haraka Nchi, Wilaya ...
Remove ads

Wilaya

Ndani ya mkoa huo kuna wilaya nane ambazo ni (katika mabano idadi ya wakazi mwaka 2022[1]):

Wakazi

Makabila makubwa huko Ruvuma ni Wangoni, Wamatengo, Wayao, Wandendeule, Wamanda, Wanyasa, Wapoto, Wabena na Wandengereko.

Karibu na Songea iko monasteri kubwa ya Peramiho ya watawa Wabenedikto na nyingine iko Hanga.

Elimu

Elimu bado inahitajika, hasa kwa maeneo ya vijijini, maana watu wengi katika mkoa huu hawajaelimika hivyo huleta changamoto katika maendeleo maana taifa huhitaji watu ambao ni wasomi.

Miundombinu

Sehemu ya mashariki ya mkoa kuna barabara ya lami kutoka Dar es Salaam kupitia Makambako na Njombe hadi Songea. Barabara kuu kwenda Lindi ni kiwango cha lami kuanzia Songea mjini kupitia Wilaya za Namtumbo, Tunduru, Nanyumbu, Masasi, Mnazimmoja-Lindi, hadi Dar es Salaam.

Majimbo ya bunge

Wakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads