Monrovia

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Monrovia ni mji mkuu wa Liberia. Kwa mujibu wa sensa ya mwaka 2008, mji huu ulikuwa na wakazi wapatao 1,021,762.

Ukweli wa haraka Nchi, - Wakazi kwa ujumla ...
Thumb
Monrovia
Thumb
Mji mkuu wa Liberia, Monrovia

Historia

Eneo uliko mji huo mwanzoni liliitwa na mabaharia Wareno Cape Mesurado walipowasilia katika miaka ya 1560. Wakati huo tayari kulikuwa na wakazi wakiishi hapo.

Mji ulianza kujengwa mwaka 1822 na chama cha American Colonization Society ikiwa ni makazi ya watu waliokombolewa toka utumwani nchini Marekani.[1] Jina Monrovia lilitokana na jina la Rais wa Marekani James Monroe.

Watu wa kwanza kuhamia Monrovia toka nchini Marekani waliwasili mwaka 1822 katika Kisiwa cha Sherboro nchini Sierra Leone. Wahamiaji wengi walifariki baada ya kuwasili Monrovia.

Mkutano wa kutunga katiba ya Liberia wa American Colonization Society ulifanyikia Monrovia mwaka 1845.

Remove ads

Uchumi

Uchumi wa Monrovia unategemea zaidi bandari yake na madini ya chuma. Bidhaa kama vile saruji, mafuta, matofali, vigae, samani, na kemikali zinatengenezwa Monrovia.

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads