Ruvuma (mto)

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ruvuma (mto)
Remove ads

Ruvuma (pia: Rovuma) ni mto mrefu wa Tanzania na Msumbiji. Mpaka kati ya Tanzania na Msumbiji unafuata mwendo wake kwa km 730.

Ukweli wa haraka Mto wa Ruvuma ...
Remove ads
Thumb
Ramani ya Mto Ruvuma

Chanzo chake kiko mashariki kwa mji wa Songea katika milima ya Matagoro upande wa mashariki wa Ziwa la Nyasa. Unaelekea magharibi kati ya vilima kwenye kimo cha mita 1000 karibu na Songea halafu unabadili mwelekeo kwenda kusini.

Unapofikia mpaka wa Tanzania na Msumbiji, takriban km 200 baada ya chanzo, unageuka tena kuelekea mashariki hadi bahari. Km 35 baada ya kuungana na mto Lujenda pana maporomoko ya Upinde.

Km 160 kabla ya kufika mdomoni bonde la Ruvuma linapanuka kuwa na upana wa km 10; lalio la mto ni karibu mita 500 likiwa na visiwa vya mchanga. Wakati wa ukame maji hupungua sana hadi watu kuvuka mto kwa miguu; wakati wa mvua umbali kati ya pande zote mbili unafikia zaidi ya kilomita moja.

Mdomo uko Bahari ya Hindi kati ya Mtwara (Tanzania) na Rasi ya Delgado (Msumbiji). Mdomo wenyewe una umbo la delta. Athira ya maji kujaa au kupwa baharini huonekana km 20 kabla ya mdomo wenyewe.

Kabla kufika kwenye delta kuna feri inayobeba magari kati ya Tanzania na Msumbiji. Feri ilipelekwa hapa na mapadre Wabenedikto wanaofanya kazi pande zote mbili za mto.

Matawimto muhimu ni mto Muhuwesi na mto Lumesule upande wa Tanzania, halafu mto Lucheringo na mto Lujenda upande wa Msumbiji.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Loading content...

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads