Nikola wa Antiokia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Nikola wa Antiokia ni Mkristo wa karne ya 1 anayejulikana hasa kutokana na Matendo ya Mitume.

Anaheshimiwa na madhehebu mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa na Kanisa Katoliki na Jumuiya Anglikana tarehe 28 Julai pamoja na wenzake Prokoro, Nikanori, Timone na Parmena [1][2].
Remove ads
Katika Biblia
Mtu wa Antiokia wa Syria, leo nchini Uturuki, alikuwa ameongokea Uyahudi kutoka Upagani. Halafu alijiunga na Ukristo akawa mmojawapo kati ya wanaume saba wa lugha ya Kigiriki katika Kanisa mama la Yerusalemu ambao, wakiwa wamejaa Roho Mtakatifu na hekima, walichaguliwa na waumini wenzao wakawekewa mikono na Mitume wa Yesu ili kushughulikia kwa niaba yao huduma za fukara (Mdo 6)[3].
Katika mapokeo
Irenei wa Lyon anasimulia[4] kwamba ndiye aliyeanzisha uzushi wa Wanikola unaolaaniwa na Ufunuo wa Yohane (2:6,15), lakini Eusebi wa Kaisarea alikanusha habari hiyo[5].
Tazama pia
Tanbihi
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads
