Prokoro mwinjilisti

From Wikipedia, the free encyclopedia

Prokoro mwinjilisti
Remove ads

Prokoro mwinjilisti ni Myahudi wa karne ya 1 anayejulikana hasa kutokana na Matendo ya Mitume.

Thumb
Mchoro wa ukutani wa Fra Angelico, ukionyesha Mtume Petro akiweka wakfu wainjilisti saba wa kwanza.

Anaheshimiwa na madhehebu mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa na Kanisa Katoliki na Jumuiya Anglikana tarehe 28 Julai pamoja na wenzake Nikanori, Timone, Parmena na Nikola wa Antiokia[1][2].

Remove ads

Katika Biblia

Alikuwa mmojawapo kati ya wanaume saba wa lugha ya Kigiriki katika Kanisa mama la Yerusalemu ambao, wakiwa wamejaa Roho Mtakatifu na hekima, walichaguliwa na waumini wenzao wakawekewa mikono na Mitume wa Yesu ili kushughulikia kwa niaba yao huduma za fukara (Mdo 6)[3].

Katika mapokeo

Mapokeo ya baadaye yanasimulia kwamba alikuwa ndugu wa Stefano, alifuatana na Mtume Petro au Mtume Yohane aliyemfanya askofu wa Nikomedia katika Uturuki wa leo.

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads