Observansya
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Observansya (kwa Kilatini: observantia, kwa Kiingereza: observantism, observant movement au observant reform) ilikuwa tapo la urekebisho lililoenea katika mashirika mbalimbali ya kitawa ya Kanisa la Kilatini kuanzia katikati ya karne ya 14 hadi katikati ya karne ya 16 au Mtaguso wa Trento (1545–1563).
Watawa hao walikusudia kushika sawasawa kanuni zao (kwa Kilatini: observantia regulae) kama ilivyokuwa mwanzoni, dhidi ya ulegevu uliosambaa kwa kawaida baada ya kifo cha waanzilishi.
Juhudi zao hazikutokana na maagizo ya Mapapa yaliyolenga kuweka mambo sawa, kama yale ya Papa Benedikto XII miaka 1335–1339.
Kati ya mashirika yaliyoguswa zaidi na tapo hilo kuna Waaugustino, Wabenedikto, Wakarmeli, Wadominiko na hasa Wafransisko.
Remove ads
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads