Papa Adeodato I

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Adeodato I
Remove ads

Papa Adeodato I (pia Adeodatus, Deodatus, Deusdedit) alikuwa Papa kuanzia tarehe 19 Oktoba 615 hadi kifo chake tarehe 8 Novemba 618[1]. Alitokea Roma, Italia[2]. Jina la baba yake lilikuwa Stephanus, ambaye alikuwa shemasi mdogo.

Thumb
Papa Adeodato I.

Alimfuata Papa Bonifasi IV akafuatwa na Papa Bonifasi V.

Kabla ya kuchaguliwa, alitoa huduma ya kipadri kwa miaka 40[3]. Alikuwa padri wa kwanza kuchaguliwa kuwa Papa tangu Yohane II mwaka 533. Baadaye alikuza idadi ya mapadri na kuwapa nafasi zilizokuwa zimeshikwa na wamonaki kadiri ya sera ya Papa Gregori I na Papa Bonifasi IV[4][3].

Kweli alijulikana kwa kupenda wakleri na waumini wake pamoja na unyofu na hekima yake [5].

Thumb
Pope Adeodatus I

Matumizi ya kwanza ya mihuri ya risasi au bullae kwenye nyaraka za Kipapa yanahusishwa naye.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[6].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[7].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads