Papa Marcellinus

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Marcellinus
Remove ads

Papa Marselino alikuwa Papa kuanzia tarehe 30 Juni 296 hadi kifo chake tarehe 25 Oktoba 304[1]. Alitokea Roma, Italia[2].

Thumb
250pix

Alimfuata Papa Kayo akafuatwa na Papa Marcellus I.

Tangu mwaka 302, Kanisa liliteseka sana chini ya Kaisari Diokletiano, aliyechochewa na kaisari Galerius. Ilisemekana kwamba Marcellinus pia aliyumba kwa muda mfupi, ila Augustino alikanusha taarifa hiyo[2].

Ikiwa Marcellino aliuawa au kufa kwa uzee, hakuna uhakika[3].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu[4].

Sikukuu yake kwa Wakatoliki ni 26 Aprili (ingawa hatajwi tena katika Martyrologium Romanum[5]) ila kwa Waorthodoksi ni tarehe 7 Juni.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads