Papa Siricius

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Siricius
Remove ads

Papa Siricius alikuwa Papa kuanzia tarehe 15 au 22 au 29 Desemba 384 hadi kifo chake tarehe 26 Novemba 399[1]. Alitokea Roma, Italia na baba yake aliiitwa Tiburtius.

Thumb
Papa Siricius.

Alimfuata Papa Damaso I[2] akafuatwa na Papa Anastasius I.

Alikuwa mtendaji na kukabili masuala mbalimbali. Amri zake 15 (hati Directa) kuhusu maisha ya Kanisa ni za kwanza kutufikia nzima bila kasoro.

Ambrosi alimsifu kama mwalimu halisi kwa sababu, akibeba mzigo wa wale wote wenye majukumu ya kiaskofu, aliwaelimisha kuhusu mafundisho ya mababu wa Kanisa, aliyoyathibitisha kwa mamlaka yake ya Kipapa pia[3].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa katika tarehe ya kifo chake[4].

Remove ads

Tazama pia

Maandishi yake

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads