Rais wa Nigeria

From Wikipedia, the free encyclopedia

Rais wa Nigeria
Remove ads

Rais wa Nigeria ni mkuu wa dola wa Shirikisho la Jamhuri ya Nigeria na kiongozi wa serikali. Vyeo vyake ni "Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Nigeria" na Amiri Jeshi Mkuu wa jeshi la Nigeria. Rais wa sasa ni Bola Tinubu.

Thumb
Rais wa Nigeria Bola Tinubu

Masharti

Kila mtu anaweza kuchaguliwa kuwa rais wa Nigeria kama

  • yeye ni raia wa Nigeria
  • umri wake ni miaka 40 au zaidi
  • ni mwanachama wa chama cha kisiasa nchini na kukubaliwa na chama hiki

Kufuatana na katiba anaweza kuhudumia awamu mbili za miaka minne akichaguliwa tena baada ya awamu ya kwanza.

Madaraka ya rais wa Nigeria

Kufuatana na katiba rais huwa na madaraka yafuatayo:

  • kukubali na kutia sahihi sheria zilizopitishwa bungeni
  • kurudisha sheria bungeni akiwa na mashaka kama sheria inalingana na katiba
  • kupeleka sheria mbele ya mahakama kuu itakayoamua kama inalingana na katiba
  • kuitisha bunge kwa makao maalumu kwa shughuli za pekee
  • kusimamika maafisa kufuatana na katiba au sheria
  • kusimamika kamati za utafiti
  • kuitisha kura ya wananchi kulingana na sheria
  • kupokea na kutambua mabalozi wa nchi za nje
  • kusimamika mabalozi
  • kusamehe wakosaji waliohukumiwa na mahakama
Remove ads

Orodha ya wakuu wa dola na maraisi wa Nigeria

Katika orodha ifuatayo kuna majina ya watu waliokuwa wakuu wa dola nchini Nigeria tangu uhuru katika mwaka 1960:

Maelezo zaidi Jina, Mwanzo ...

Viungo vya Nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads