Yombeyombe

From Wikipedia, the free encyclopedia

Yombeyombe
Remove ads

Yombeyombe au yombiyombi ni ndege wadogo wa familia mbalimbali. Spishi moja iko katika Ploceidae, moja katika Viduidae na 24 katika Fringillidae. Hawa ni ndege wanene yenye domo nene na rangi mbalimbali kama nyeusi, kahawia, njano na nyekundu kufuatana na spishi. Wanatokea misitu na maeneo mengine yenye miti au matete (yombeyombe wa kawaida). Hula mbegu lakini hulisha makinda yao wadudu. Yombeyombe wa kawaida hulifuma tago lake kwa majani ya manyasi katikati ya matete au mafunjo au pengine katika kichaka. Jike huyataga mayai 2-5. Yombeyombe wa Fringillidae hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika panda ya mti na jike huyataga mayai 2-7. Tofauti na yombeyombe wengine yombeyombe manjano hajengi tago lake mwenyewe lakini jike huyataga mayai katika matago ya spishi nyingine, k.m. spishi za videnenda na magamaga.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Spishi za Afrika

Familia Ploceidae

  • Amblyospiza albifrons, Yombeyombe (Grosbeak au Thick-billed Weaver)

Familia Viduidae

  • Anomalospiza imberbis, Yombeyombe Manjano (Cuckoo-finch au Parasitic Weaver)

Familia Fringillidae

Remove ads

Spishi za mabara mengine

Familia Fringillidae

Remove ads

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads