Seaborgi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Seaborgi (kwa Kiingereza: seaborgium) ni elementi sintetiki iliyo na alama Sg na namba atomia 106. Imepokea jina lake kwa heshima ya mwanakemia wa Marekani Glenn T. Seaborg . Ilhali ni elementi sintetiki, haitokei kiasili katika mazingira yetu lakini inaweza kuundwa katika maabara. Ni dutu nururifu; isotopi yake iliyo thabiti zaidi inaitwa 269 Sg, ikiwa na nusumaisha ya dakika 14 hivi.
Atomu za kwanza za seaborgi zilitengenezwa mwaka 1974 katika maabara huko Umoja wa Kisoyeti na Marekani. Pande hizo mbili zilivutana kwa miaka kadhaa kuhusu nani aliwahi kuigundua na haki ya kuamulia jina, hadi mwaka 1997 Jumuiya ya Kimataifa ya Kemia (IUPAC) iliamua jina rasmi kuwa "seaborgium".
Tabia nyingi za elementi hiyo hazijulikani kwa sababu mbili
a) elementi hii inapatikana tu baada ya kutengenezwa katika maabara kwa gharama kubwa [1]
b) baada ya kupatikana inaachana haraka, haidumu

Remove ads
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads