T-Pain
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Faheem Rasheed Najm (anafahamika zaidi kwa jina la kisanii kama T-Pain; amezaliwa 30 Septemba 1985) ni mwimbaji, mtunzi, rapa, na mtayarishaji wa rekodi kutoka Marekani.
Remove ads
Wasifu
Najm alizaliwa mjini Tallahassee, Florida.[1] Jina lake la kisanii ni kifupi cha "Tallahassee Pain" ("Tallahassee Mauimivu) na amechagua jina hilo kwa sababu ya ugumu wa maisha aliyoyapata wakati anaishi huko.[2]
Alianza shughuli za urapa akiwa katika kundi la Nappy Headz. Mnamo mwaka wa 2005, akawa mwimbaji na kuweza kutoa albamu yake ya kwanza iliyoitwa Rappa Ternt Sanga ikiwa na vibao vyake vikali vya "I'm Sprung" na "I'm N Luv (Wit A Stripper)".
Shughuli zake kama mwimbaji, T-Pain ametumia sana kionjo cha sauti cha Auto-Tune. Tangu kutolewa kwa albamu yake ya kwanza, T-Pain ametayarisha vibao kadhaa vikali vyake mwenyewe na vya marapa na waimbaji wengine wa R&B. T-Pain pia amekuwa na single kumi kwenye chati za Billboard Hot 100. Mnamo mwaka wa 2008, ameshinda tuzo ya Grammy na rapa Kanye West kwa ajili ya single ya "Good Life". Mnamo mwaka wa 2010 ameshinda tuzo nyingine ya Grammy na Jamie Foxx kwa ajili ya single ya "Blame It". T-Pain pia ni mwanzilishi wa studio ya kurekodia ya Nappy Boy Entertainment, imeanzishwa mwaka wa 2005.
Remove ads
Kazi
Diskografia
- Rappa Ternt Sanga (2005)
- Epiphany (2007)
- Thr33 Ringz (2008)
- RevolveR (2010)
- Single zake
- "Bring It Back" ft. Chris Brown (2016)
- "Thing Now" ft. TryBishop (2016)
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads