Thomas Becket

From Wikipedia, the free encyclopedia

Thomas Becket
Remove ads

Thomas Becket (Cheapside, London, Uingereza, 1118 (au 1120) 29 Desemba 1170) alikuwa Askofu mkuu wa Canterbury tangu 1162 hadi kifodini chake kilichotokea wakati wa Misa katika kanisa kuu.

Thumb
Mchoro mdogo katika kitabu cha Zaburi cha Uingereza, 1250 hivi, Walters Art Museum, Baltimore, Marekani.

Sababu ya kuuawa ni kubishana kwake na mfalme Henri II wa Uingereza juu ya haki na juu ya fadhili za Kanisa.

Kwa ajili hiyo alikuwa ameshafukuzwa kutoka jimbo lake na kutoka ufalme wote wa Uingereza.

Baada ya miaka sita aliweza kurudi nchini, lakini aliendelea kusumbuliwa sana hadi alipomuendea Kristo kwa kuchomwa na askari wa mfalme kwa upanga [1].

Muda mfupi baadaye Papa Alexander III alimtangaza mtakatifu mfiadini tarehe 21 Februari 1173. Ndivyo anavyoheshimiwa na Kanisa Katoliki na Anglikana.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 29 Desemba[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads