Timotheo
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Timotheo (labda Listra, 17 hivi - Efeso, 97) ni mfuasi mpendwa wa Mtume Paulo, halafu mwandamizi wake [1].


Paulo alimuandikia barua mbili zilizopokewa katika Biblia kati ya Nyaraka za Kichungaji. Habari zake tunazipata humo na katika Matendo ya Mitume.
Tangu kale anaheshimiwa kama askofu mtakatifu na Wakatoliki na Waorthodoksi.
Tangu mwaka 1969, Kanisa Katoliki la Kilatini linamwadhimisha pamoja na Tito tarehe 26 Januari, siku inayofuata ile ya Uongofu wa Mt. Paulo, mwalimu wao.[2][3][4]. Waorthodoksi wanamuadhimisha tarehe 22 Januari.
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo ya Kiswahili
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads