Hamed bin Mohammed el Murjebi
Mfanyabiashara wa Utumwa From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Hamad bin Muhammad bin Juma bin Rajab el Murjebi (amejulikana zaidi kwa jina la Tippu Tip; 1837 – 14 Juni 1905) alikuwa mfanyabiashara mashuhuri katika Afrika ya Mashariki na ya Kati wakati wa karne ya 19.
Remove ads
Alikutana na wapelelezi mashuhuri kama David Livingstone, Henry Morton Stanley na Hermann von Wissmann.
Kwa miaka kadhaa alikuwa gavana wa Kongo ya Mashariki kwa niaba ya mfalme wa Ubelgiji.
Alitunga tawasifu kuhusu maisha yake.
Remove ads
Mfanyabiashara
Baba yake alikuwa mfanyabiashara Mwarabu Muhammed bin Juma, mama yake Bint Habib bin Bushir, alikuwa Mwarabu wa tabaka la watawala toka Muscat.
Hamed aliingia katika shughuli za biashara tangu umri wa miaka 12 akafaulu katika biashara ya misafara kati ya Zanzibar na Kongo.
Akiwa na umri mdogo, Hamad aliongoza kundi la wanaume 100 kwenda Afrika ya Kati kutafuta watumwa na pembe za ndovu.[1] Baada ya kuvamia maeneo mengi alirudi Zanzibar kuimarisha vyanzo vyake na kukusanya watu wa kumsaidia ili arudi bara.[2] Hapa alipokea jina la Tippu Tip. Kwa mujibu wake mwenyewe, jina hilo lilitokana na mlio wa bunduki yake wa 'tiptip. [3]
Alipanga misafara ya mahamali waelfu akipeleka bidhaa kutoka Bagamoyo kupitia Tabora hadi Ujiji kwa Ziwa Tanganyika na ndani ya Kongo. Bidhaa alizobeba alizitumia kujipatia pembe za ndovu na watumwa; watumwa walisaidia kubeba pembe za ndovu njia ya kurudi hadi pwani. Hamed alitajirika sana. Athira yake ilipanuka katika Kongo ya Mashariki hadi alitawala eneo kubwa sana.
Remove ads
Kukutana na wapelelezi Wazungu
Hamed akapata jina huko Ulaya kwa sababu alikutana na wasafiri na wapelelezi Wazungu kama David Livingstone, Veney Cameron, Henry Morton Stanley, Eduard Schnitzer (Emin Pascha), Hermann von Wissmann na Wilhelm Junker ambao mara nyingi walipata misaada muhimu kutoka kwake.[4] Kati ya mwaka 1884 na 1887 alikuwa mtu mwenye mamlaka katika sehemu kubwa za Mashariki ya Kongo.
Gavana wa Mfalme wa Ubelgiji
Wabelgiji walipoanza kujenga ukoloni wao Kongo walimkuta kama mtawala wa Kongo ya Mashariki wakapatana naye na kumpa cheo cha gavana ya Mkoa wa Chutes Stanley ("maporomoko ya Stanley", leo Kisangani) mwaka 1887 alichoshika kwa miaka michache.
Mwanzoni mwa 1887, Stanley aliwasili Zanzibar na kumtaka Hamad awe gavana wa Wilaya ya Stanley Falls kwenye Dola Huru la Kongo, iliyokuwa koloni binafsi la mfalme wa Ubelgiji. Mfalme Leopold II wa Ubelgiji na Sultani Barghash bin Said wa Zanzibar walikubaliana na tarehe 24 Februari 1887, Hamad alikubali. Wakati huohuo alikubali kuongoza safari za Stanley ili kwenda kumuokoa Mjerumani Emin Pasha (E. Schnitzer), gavana wa Kiosmani wa Equatoria (eneo la Misri ya Kiosmani, Sudan Kusini ya leo).

Kurudi Zanzibar
Mabadiliko ya ukoloni yaliharibu biashara yake akarudi Zanzibar 1890/1891 alipobaki bila misafara mipya hadi kifo chake mwaka 1905.
Hamed amejipatia nafasi katika historia ya Afrika ya Mashariki kwa kuandika yeye mwenyewe tawasifu au kumbukumbu ya maisha yake. Katika lugha ya Kiswahili ndio mfano wa kwanza wa tawasifu. Pia ni mfano wa pekee wa kumbukumbu ya kimaandishi ya matokeo ya siku zile zisizoandikwa na Mzungu lakini na mwenyeji. Aliandika kwa lugha ya Kiswahili akitumia mwandiko wa Kiarabu. Mfasiri katika Ukonsuli wa Ujerumani kwenye kisiwa, Heinrich Brode alinakili muswada wake kwa herufi za Kilatini na kuongeza tafsiri ya Kijerumani iliyochapishwa huko Berlin katika sehemu mbili mwaka 1902 na 1903 [5], [6] .
Brode alitumia kazi hiyo kutunga kitabu chake juu ya Hamed kilichochapishwa mwaka 1905 na kutafsiriwa kwa Kiingereza mwaka 1907[7].
Remove ads
Vita ya Waarabu katika Kongo na kuporomoka wa urithi wa Tippu Tip
Baada ya kuondoka kwake Hemed katika Kongo, vita ya Waarabu katika Kongo ilianza. Waarabu na Waswahili wa Kongo Mashariki walipigana na serikali ya kikoloni ya Dola Huru la Kongo ilhali pande zote mbili zilitumia askari Waafrika wengi walioongozwa na viongozi wa nje, ama Waarabu /Waswahili au Wazungu.
Tippu Tip alipoondoka Kongo, uwezo wa Dola Huru la kikoloni la Mfalme Leopold bado ulikuwa hafifu sana katika sehemu za mashariki. Mamlaka ilikuwa mkononi mwa Waarabu au Waswahili waliofanya biashara ya pembe za ndovu na watumwa kwenda Zanzibar. Kati yao walikuwa Sefu bin Hamed, mwana wa Tippu Tip, na mfanyabiashara aliyejulikana kwa jina la Rumaliza katika maeneo upande wa magharibi ya Ziwa Tanganyika.
Mwaka 1892 Sefu bin Hamed alishambulia Wabelgiji waliofanya biashara ya pembe za ndovu iliyokuwa hatari kwa biashara ya Waswahili. Serikali ya koloni ya Dola Huru la Kongo ilituma kikosi chini ya kamanda Francis Dhanis kwenda sehemu za mashariki. Dhanis alifaulu mapema kushawishi kiongozi Mwafrika Ngongo Lutete aliyewahi kushirikiana na Sefu ahamie upande wake. Jeshi lake lilikuwa na silaha bora na nidhamu bora kati ya askari wake, likafaulu kumshinda Sefu mara kadhaa hadi ifo chake kwenye Oktoba 1893. Kutoka hapa Dhanis aliendelea kumshambulia Rumaliza na hatimaye kumlazimisha akimbie katika eneo la Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.
Kwa njia hii Wabelgiji walifaulu kuvunja nguvu ya Waarabu na Waswahili katika Kongo Mashariki. Kisiasa hakuna kitu kilichobaki na juhudi za Hemed bin Mohammed el Murjebi kujenga milki yake katika Kongo, ila tu kiutamaduni Hemed na wenzake walifaulu kueneza lugha ya Kiswahili katika sehemu zile.
Remove ads
Kifo
Hamad alifariki kutokana na ugonjwa wa malaria tarehe 13 Juni 1905 katika nyumba yake kwenye Mji Mkongwe wa Zanzibar.
Jina lake linajulikana kama mfano wa mabaya ya biashara ya watumwa iliyoharibu maeneo makubwa huko Kongo kabla ya mwanzo wa ukoloni. Yeye mwenyewe aliona watumwa ni sehemu tu ya biashara yake akitajirika hasa na biashara ya pembe za ndovu.
Marejeo
Vyanzo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads