Yohane wa Dukla

From Wikipedia, the free encyclopedia

Yohane wa Dukla
Remove ads

Yohane wa Dukla (kwa Kipolandi: Jan z Dukly; Dukla, Polandi, 1414 - Lviv, leo nchini Ukraina, 1484 [1]) alikuwa mtawa na padri wa shirika la Ndugu Wadogo [2]

Thumb
Mt. Yohane wa Dukla.

Maisha

Ingawa alijiunga kwanza na Ndugu Wadogo Wakonventuali, baadaye akahamia urekebisho wa Observansya akaishi maisha ya sala na juhudi za kiroho, lakini pia alifanya kwa ari uchungaji na kulenga umoja wa Wakristo[3].

Hata baada ya kupofuka aliendelea kuandaa hotuba zake maarufu kwa kurudisha watu wengi kwenye Kanisa.[1]

Heshima baada ya kifo

Mara baada ya kifo chake aliheshimiwa kama mtakatifu na miujiza mbalimbali ilisemekana kutokea kaburini pake.

Hatimaye, tarehe 10 Juni 1997, Papa Yohane Paulo II alimtangaza rasmi kuwa mtakatifu katika misa aliyoadhimisha huko Krosno, Poland, wakishiriki watu milioni 1 hivi.

Sikukuu yake ni tarehe 29 Septemba[4].

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads