Yosefu Mtungatenzi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Yosefu Mtungatenzi
Remove ads

Yosefu mtungatenzi (Sicilia, Italia, 816 - Konstantinopoli, leo nchini Uturuki, 3 Aprili 886) alikuwa mmonaki padri katika monasteri ya Thesalonike, Ugiriki.

Thumb
Picha takatifu ya Mt. Yosefu mtungatenzi.

Ni maarufu hasa kwa tenzi zake zinazotumika hadi leo hata katika Ukristo wa Magharibi ambazo zimemfanya mmojawapo kati ya watunzi wakuu wa muziki wa Kikristo[1].

Alidhulumiwa sana na serikali kwa kutetea heshima kwa picha takatifu. Kwa ajili hiyo alitumwa pia Roma kuomba ulinzi wa Papa.

Hatimaye alikabidhiwa utunzaji wa vyombo vitakatifu vya kanisa la Hagia Sophia[2].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu[3].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Aprili[4].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads