Ndege wakubwa kiasi wa jenasi Coua, familia Cuculidae From Wikipedia, the free encyclopedia
Kua (kutoka Kimalagasy: koa) ni ndege wakubwa kiasi wa jenasi Coua katika nusufamilia Phaenicophaeinae ya familia Cuculidae. Pengine wanaainishwa katika nusufamilia yao Couinae pamoja na kekeo-ardhi wa Asia (Carpococcyx). Jenasi pekee ya Bara la Afrika inayoainishwa katika Phaenicophaeinae ni Ceuthmochares (ukiki). Kua ni ndege wa Madagaska wanaofanana na kekeo. Wana mkia mrefu na miguu mirefu. Kidole cha tatu cha miguu yao kinaweza kukabili mbele au nyuma. Rangi kuu ni kijivu na/au buluu na wana ngozi tupu kuzunguka macho yenye rangi buluu. Kua hula mbegu, matunda madogo, wadudu na wanyama wadogo kama mijusi na vigeugeu. Kinyume na kekeo, kua hulijenga tago lao lenyewe. Jike huyataga mayai meupe 1-3 (2 mara nyingi zaidi).
Kua | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Kua mkubwa | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Spishi 11:
| ||||||||||||||
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.