Malkoha

Ndege wasio vidusia wa familia Cuculidae From Wikipedia, the free encyclopedia

Malkoha
Remove ads

Malkoha (kutoka Kisinhala: mal-koha au kekeo-maua) ni ndege wakubwa kiasi wa nusufamilia Phaenicophaeinae katika familia Cuculidae. Spishi za malkoha zinazotokea Afrika zinaitwa ukiki (Ceuthmochares) na kua (Coua) kwa Kiswahili. Lakini hivi karibuni wataalamu wengine wameainisha kua katika nusufamilia yao, Couinae, pamoja na kekeo-ardhi (Carpococcyx). Nje ya Afrika spishi zote zinatokea misitu ya Asia ya Kusini na ya Mashariki. Rangi za ndege hawa ni kijivu, kahawia au buluu, pengine nyeupe chini, na spishi nyingi zina nyekundu kwa tumbo, koo, uso, kishungi na/au domo. Spishi zinazotafuta chakula ardhini zina miguu yenye nguvu na zinaweza kukimbia. Zile zinazokaa mitini huenda kutoka tawi hadi tawi na kuruka kama dudumizi. Hula wadudu na vertebrata wadogo kama mijusi hasa lakini mbegu na beri pia. Kinyume na kekeo (Cuculinae) malkoha hutengeneza tago lao lenyewe katika mti kwa kawaida. Jike hutaga mayai 1-5 kufuatana na spishi.

Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Remove ads

Spishi za Afrika

Remove ads

Spishi za Asia

Remove ads

Picha

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads