From Wikipedia, the free encyclopedia
New Delhi (yaani Delhi Mpya; kwa Kihindi: |नई दिल्ली, kwa Kiurdu: نئی دلی) ni mji mkuu wa Uhindi na kitovu cha jiji kubwa la Delhi. Pamoja na Delhi yote kuna wakazi zaidi ya milioni kumi.
Jiji la New Delhi | |
Mahali pa New Delhi katika Uhindi |
|
Majiranukta: 28°40′0″N 77°13′0″E | |
Nchi | Uhindi |
---|---|
Tovuti: http://www.ndmc.gov.in/ |
Iko kaskazini mwa nchi kwenye kingo za mto Yamuna katika tambarare ya bonde la Ganga. Mji huo uko m 216 juu ya UB kwa wastani.
Delhi ina historia ndefu sana iliyoanza mnamo mwaka 1200 KK. Iliharibiwa mara nyingi na kujengwa upya na kubadilisha jina pamoja na wakazi na watawala wake. Katika karne zilizopita ilikuwa mji mkuu wa Dola la Moghul na tangu mwaka 1911 wa Uhindi wa Kiingereza.
Delhi Mpya ilianzishwa baada ya azimio la George V, mfalme wa Uingereza na Kaisari wa Uhindi, la kuhamisha mji mkuu kutoka Kolkata kwenda Delhi. Mji mpya ulijengwa kando ya Delhi ya Kale na kukabidhiwa mwaka 1931. Ulisanifiwa na wasanifu Waingereza Edwin Lutyens (1869-1944) na Herbert Baker (1862-1946).
Tangu mwaka 1947 New Delhi ni mji mkuu wa Uhindi huru.
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu New Delhi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.