Adalbert wa Magdeburg

From Wikipedia, the free encyclopedia

Adalbert wa Magdeburg
Remove ads

Adalbert wa Magdeburg (alifariki 20 Juni, 981) alikuwa mmisionari na askofu mkuu wa kwanza wa mji wa Magdeburg, Ujerumani.

Thumb
Mtakatifu Adalbert wa Magdeburg

Tangu kale ametambuliwa kuwa mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 20 Juni[1].

Maisha

Adalbert alizaliwa Ujerumani na kuwa mtawa katika monasteri ya Wabenedikto wa mji wa Trier.

Baada ya kuwekwa wakfu kama askofu, mwaka 961 alitumwa mjini Kiev (Ukraine) kama mmisionari.

Kundi lake lote liliuawa, naye peke yake aliweza kurudi Ujerumani.

Baadaye aliteuliwa kuwa askofu mkuu wa dayosisi ya Magdeburg.

Alianzisha madayosisi mapya mengi upande wa Mashariki wa Ujerumani, kama katika miji ya Naumburg, Meisen, Merseburg, Brandenburg, Havelberg, na Poznan.

Mwanafunzi wake mmoja aliyetangazwa kuwa mtakatifu kama yeye ni Adalbert wa Praha.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads