Adalbert wa Prague

From Wikipedia, the free encyclopedia

Adalbert wa Prague
Remove ads

Adalbert wa Prague (kwa Kicheki Vojtěch, kwa Kipolandi Wojciech, kwa Kijerumani Adalbert, jina alilojichagulia alipopewa Kipaimara na Adalbert wa Magdeburg ; Libice, leo nchini Ucheki 956 hivi – Tenkitten, leo nchini Urusi, 23 Aprili 997) alikuwa askofu wa Prague (Ucheki) tangu mwaka 983.

Thumb
Mt. Adalbert wa Prague.
Thumb
Fuvu la kichwa chake.
Thumb
Masalia katika sanduku la fedha katika kanisa kuu, Gniezno, Polandi.

Huko alipatwa na matatizo mengi akafanya safari nyingi kwa jina la Kristo, akijitahidi kwa nguvu zote kung'oa desturi za Kipagani. Alipotambua kwamba matunda yake ni machache, alikwenda Roma akawa mmonaki Mbenedikto.

Hatimaye alikwenda Polandi ili kuwaletea imani Waprusia, akachomwa kwa mikuki na Wapagani kadhaa[1].

Mwaka 999 alitangazwa na Papa Silvesta II kuwa mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake ni tarehe 23 Aprili[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads