Al-Shabaab

From Wikipedia, the free encyclopedia

Al-Shabaab
Remove ads

Kuhusu Al-Shabaab nchini Msumbiji tazama Ansar al-Sunna Msumbiji

Thumb
Bendera ya Al-Shabaab.

Al-Shabaab (kwa Kiarabu: الشباب, "Vijana"; kirefu: حركة الشباب المجاهدين, Ḥarakat ash-Shabāb al-Mujāhidīn; kifupisho: HSM; kwa Kisomali: Xarakada Mujaahidiinta Alshabaab; maana yake "Tapo la Vijana wa Jihad") ni kundi la Waislamu wenye itikadi kali lililoanzishwa nchini Somalia mwaka 2006 kutokana na Islamic Courts Union (ICU)[1].

Mwaka 2012 lilijiunga na Al-Qaeda.[2][3][4][5].

Wanamgambo wa Al-Shabaab walikadiriwa kuwa 7,000 - 9,000 mwaka 2014, wakiwemo wageni wengi, hasa kutoka Yemen, Sudan, Kenya, Tanzania, Afghanistan, Saudi Arabia, Malaysia, Pakistan na Bangladesh[6].

Mwaka 2015 waliacha miji yote muhimu na kuendelea kutawala maneno machache ya vijijini tu.[7]

Hata hivyo wanaendelea kupigana na wanaotazamwa nao kama maadui wa Uislamu hasa nchini Somalia, Kenya na Yemen. Kundi linaloitwa Al-Shabaab nchini Msumbiji lilianzishwa kwa njia tofauti, si tawi la Al-Shabaab wa Somalia.

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads