Somalia

nchi huru barani Afrika From Wikipedia, the free encyclopedia

Somalia
Remove ads

Somalia (kwa Kisomali: Soomaaliya; jina rasmi: Jamhuri ya Shirikisho ya Somalia) ni nchi katika Afrika ya Mashariki, iliyoko kwenye Pembe ya Afrika. Inapakana na Ethiopia magharibi, Jibuti kaskazini-magharibi, Kenya kusini-magharibi, na imezungukwa na Bahari ya Hindi mashariki. Ina idadi ya watu takriban milioni 18.1, ikiwa ya 78 duniani. Jiji lake kubwa zaidi na mji mkuu ni Mogadishu. Somalia imegawanyika katika majimbo sita ya shirikisho. Inajulikana kwa pwani yake ndefu zaidi barani Afrika na kwa changamoto zake za kisiasa na kiusalama kutokana na miongo ya migogoro ya ndani.

Ukweli wa haraka Jamhuri ya Somalia Jamhuuriyadda Federaalka Soomaaliya, Mji mkuu na mkubwa ...

Somalia ina historia ndefu na utamaduni, ikiwa ni mojawapo ya maeneo ya kale yaliyojihusisha na biashara ya majini katika Bahari ya Hindi. Katika enzi za zamani, miji ya pwani kama Mogadishu, Berbera, na Zeila ilikuwa vituo muhimu vya biashara kati ya Afrika, Uarabuni, na Asia. Somalia pia ni maarufu kwa utamaduni wake wa kisanaa, mashairi, na lugha ya Kisomali ambayo ni mojawapo ya lugha za Kiafrika zenye sarufi ya kipekee na utajiri wa fasihi.

Licha ya changamoto za kiusalama, hivi karibuni Somalia imeonyesha dalili za kuimarika katika nyanja mbalimbali kama elimu, miundombinu, na biashara, hasa katika maeneo yenye utulivu kama Somaliland na Puntland. Jumuiya ya kimataifa pamoja na mashirika ya ndani yamekuwa yakishirikiana katika juhudi za ujenzi wa taifa na kukuza utawala bora. Aidha, wimbi la watu wa Somalia walioko ughaibuni (diaspora) limechangia kwa kiasi kikubwa maendeleo kupitia uhamishaji wa fedha, uwekezaji, na maarifa.

Remove ads

Jiografia

Makala kuu: Jiografia ya Somalia
Thumb
Ramani ya mikoa ya Somalia.

Historia

Thumb
Mji wa Bosaso, Somalia.

Ukoloni wa Italia

Kuanzia mwaka 1888 Italia ilijipatia mikataba ya ulinzi na masultani mbalimbali waliotawala maeneo madogo kwenye Pembe ya Afrika. Walitangulia 1889 na sultani ya bandari ya Hobyo na mtawala wa usultani wa Majerteen.

Mwaka 1892 Usultani wa Zanzibar ulikodisha bandari ya Banadir kati ya Mogadishu hadi Brava kwa Italia. Mwaka 1905 Italia ilinunua eneo hili kutoka Zanzibar na kulitangaza kuwa koloni na Mogadishu kuwa mji mkuu.

Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Waitalia walikabidhiwa na Uingereza eneo la Kismayu. Walilitawala kwa jina la "Oltre Giuba" (ng'ambo ya mto Juba) na kuliunganisha na Somalia ya Kiitalia tarehe 30 Juni 1926.

Wakati uleule waliamua kumaliza hali ya sultani za Majarteen na Hobyo kuwa nchi lindwa na kuzifanya sehemu kamili za koloni. Mipango hiyo ilisababisha vita kali ya miaka miwili kwa sababu masultani waliona mikataba yao ya ulinzi ilivunjwa wakapinga jeshi la Italia.

Mwaka 1936 Somalia ikaunganishwa na Ethiopia kuwa sehemu ya Afrika ya Mashariki ya Kiitalia.

Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia makoloni ya Italia yalivamiwa na Uingereza uliotawala Somalia tangu 1941.

Mwaka 1949 Somalia ilirudishwa mikononi mwa Italia ilisimamie kwa niaba ya Umoja wa Mataifa.

Ukoloni wa Uingereza

Uingereza uliingia katika eneo hili baada ya Misri kuondoka mwaka 1885 kwa kushindwa na jeshi la Mahdi huko Sudan. Uingereza uliingia kwa sababu iliona umuhimu wa kutawala pande zote mbili za Bab el Mandeb ikihofia uenezaji wa nchi nyingine za Ulaya, hasa Ufaransa iliyokuwa na koloni la kwanza ya Ubuk (Obok) katika Jibuti ya leo tangu 1862. Pamoja na hayo Waingereza walitegemea kununua nyama kwa ajili ya mji wa Aden na meli zilizopita hapo kati ya Uhindi na Ulaya.

Somaliland ilitawaliwa awali kama mkoa wa Uhindi wa Kiingereza ikawa baadaye chini ya wizara ya makoloni huko London.

Thumb

Hata kama Uingereza haukuwa na nia ya kuingilia mno maisha ya wenyeji ulikutana na upinzani mkali kuanzia mwaka 1899 kutoka kwa kiongozi wa dini Diiriye Guure, aliyeitwa na Waingereza "Mullah majununi". Waingereza walijibu kwa ukatili katika vita vya miaka 20 iliyoua takriban theluthi moja ya wakazi wote wa eneo.

Mwishowe Uingereza iliweza kumaliza upinzani kwa teknolojia mpya ya eropleni za kijeshi zilizotumia mabomu na bunduki za mtombo kutoka angani kwa mara ya kwanza katika Afrika.

Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia eneo likatwaliwa na Italia katika Agosti 1940 lakini lilichukuliwa tena na Uingereza katika Machi 1941.

Uhuru

Mwaka 1960 utawala wa kikoloni ulikwisha na Somalia ikapata uhuru wake, ikiunganisha makoloni mawiliː la Waitalia (kusini) na la Waingereza (kaskazini).

Baada ya mwaka 1991 nchi ya Somalia ilibaki haina serikali wala umoja wa taifa, bali iligawiwa na wakereketwa na wanamgambo wa ukoo na eneo, hasa Somaliland, Puntland na Galmudug upande wa kaskazini.

Katika miaka 2008-2013 ilihesabika kama nchi filisika. Kwa sasa ni nchi dhaifu lakini inaanza kujengwa upya kama shirikisho na kujiandaa kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Tarehe 4 Machi 2024 imejiunga rasmi na Jumuia ya Afrika Mashariki[1].

Thumb
Klipspringers anaishi katika maeneo ya milimani yenye mimea kidogo.
Remove ads

Watu

Tazama pia: Orodha ya lugha za Somalia

Thumb
Hii ramani ya mwaka 2002 inaonyesha msongamano wa watu nchini.

Wakazi asili wa Somalia ni Wasomali (85%) wa makabila yafuatayo:

    • Isaaq
    • Hawiye
    • Dir
    • Darod
    • Digil & Mifle

Wengine (15%) ni:

Thumb
Ramani ikionyesha uenezi wa lugha ya Kisomali katika Pembe la Afrika.

Kisomali ndiyo lugha ya kawaida ya wakazi wengi na lugha rasmi pamoja na Kiarabu. Kati ya lugha nyingine zinazotumika nchini, mojawapo ni Kiswahili (lahaja za Chimbalanzi na Kibajuni).

Upande wa dini, 99.8% ni Waislamu, hasa Wasuni. Wakristo hawafikii 0.1%.

Thumb
Somali lahoh (canjeero).
Thumb
Maporomoko ya maji ya Lamadaya kwenye mlima Cal Madow.
Thumb
Eneo la Somaliland.
Thumb
Mandhari ya milima ya Cal Madow, makao ya spishi nyingi za pekee.
Thumb
Ufukwe wa Berbera.
Thumb
Dahabshiil huko Hargeisa.
Thumb
Duka huko Burao.
Thumb
Hargeisa International Airport huko Hargeisa.
Thumb
Watu mjini Hargeisa.

Utawala

Maeneo (umoja: gobolka, wingi: gobollada) ya Somalia, ambayo imegawiwa tena katika wilaya, ni 18:

Maelezo zaidi Mkoa, Eneo (km2) ...
Thumb
Banda la biashara huko Mogadishu.
Remove ads

Mawasiliano

Mawasiliano ya Jamhuri ya Somalia ilikaribia kuangamia kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe, lakini kwa sasa kampuni za binafsi za mawasiliano ya mitambo, zimetwaa karibu miji yote Somalia, na hata kutoa huduma njema kuliko nchi zilizo jirani.

Somalia ni nchi mojawapo Afrika ambayo ina mawasiliano ya bei rahisi zaidi, pengine kwa kuwa Somalia haikuwa na serikali iliyotoza ushuru; (Telecoms thriving in lawless Somalia) Kampuni zinazohudumia watu wa Somalia ni kama:

  • SOMTEL
  • Galkom
  • Global Internet Company
  • Hormuud
  • Telcom
  • Nationlink
  • Netco
  • STG
  • Dahabshiil
Remove ads

Tazama pia

Remove ads

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads