Ana Schaeffer

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ana Schaeffer
Remove ads

Ana Schaeffer (Mindelstetten, Bavaria, Ujerumani, 18 Februari 1882 – Mindelstetten, 5 Oktoba 1925), alikuwa mwanamke mwenye karama za pekee katika maisha ya ugonjwa[1] nyumbani akizama katika sala.

Thumb
Picha halisi ya Mt. Ana.

Ni kwamba, alipokuwa na umri wa miaka 19, akiwa mfanyakazi wa ndani, alimwagikiwa maji ya moto, tukio lililozidi kuathiri vibaya afya yake; hata hivyo aliishi kwa utulivu katika ufukara, akimtolea Mungu msalaba wa maumivu yake kwa ajili ya wokovu wa watu[2].

Mwaka 1910 alijikuta ana madonda mwilini kama yale ya Yesu msulubiwa[3]. Pia alipata njozi.

Alitangazwa na Papa Yohane Paulo II kuwa mwenye heri tarehe 7 Machi 1999[4], halafu Papa Benedikto XVI alimtangaza mtakatifu tarehe 21 Oktoba 2012[5].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 5 Oktoba[6].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads