Eugenius wa Karthago

From Wikipedia, the free encyclopedia

Eugenius wa Karthago
Remove ads

Eugenius wa Karthago (alifariki 13 Julai 505) alikuwa Mkristo aliyechaguliwa kwa kauli moja kuwa askofu wa mji huo mwaka 480 baada ya Deogratias wa Karthago (aliyefariki 456).

Thumb
Sanamu yake iliyoko Milano, Italia.

Ilimbidi atetee imani sahihi kwa kupambane na Uario, ulioungwa mkono na mfalme wa Wavandali. Alifaulu kuwavuta baadhi yao katika Kanisa Katoliki na kwa sababu hiyo alifukuzwa akaishi uhamishoni katika jangwa la Libia [1].

Halafu aliruhusiwa kurudi, lakini miaka minane baadaye akafukuzwa tena ahamie Vienne, karibu na Albi (leo nchini Ufaransa). Huko alijenga monasteri aliposhika maisha ya toba hadi kifo chake[2].

Kutokana na imani na maadili yake, tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu na babu wa Kanisa.

Sikukuu yake inaadhimishwa tarehe 13 Julai[3].

Remove ads

Maandishi

  • Expositio Fidei Catholicae
  • Apologeticus pro Fide
  • Altercatio cum Arianis.[4]

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads