Gaudioso wa Napoli

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Gaudioso wa Napoli (jina kamili kwa Kilatini: Septimius Celius Gaudiosus; pia: Sanctus Gaudiosus Africanus, yaani Mtakatifu Gaudioso Mwafrika; 385 - 455) alikuwa askofu wa Abitine, karibu na Karthago, leo nchini Tunisia.

Mwaka 439 alikimbia Afrika Kaskazini wakati wa dhuluma za Genseriki, mfalme wa Wavandali, dhidi ya Wakatoliki akahamia Napoli pamoja na askofu wa Karthago, Quodvultdeus, na wengineo.

Alifariki kitakatifu monasterini. Inasadikika kwamba ndiye aliyeingiza huko kanuni ya Augustino wa Hippo.[1][2]

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 27 Oktoba[3].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads