Isimila
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Isimila ni eneo la kihistoria lililopo katika kijiji cha Ugwachanya, kata ya Mseke, mkoani Iringa nchini Tanzania, kilomita 20 kutoka Iringa mjini karibu na barabara kuu ya A 104 kuelekea Mbeya.
Njia ya kuingia si rahisi kuikuta: ukitokea Iringa iko kabla ya kufikia Tanangozi, upande wa kushoto.
Eneo hili ni kivutio kimojawapo kinachoupamba mkoa wa Iringa.
Bonde la Isimila lilikaliwa na watu tangu Zama za Mawe za Kale. Ni katika eneo hilo ndipo zana za mawe za kale na nguzo za asili za Isimila zilipogunduliwa tangu mwaka 1951.
Zana hizo zinasadikiwa kuwa zilikuwepo tangu miaka 260,000 kabla ya Kristo, umri uliopatikana kwa kupimwa mifupa ya kibinadamu iliyokutwa kati ya mawe yaliyochongwa kama zana[1].
Miongoni mwa zana zilizopo katika korongo la Isimila, ambalo lina mikondo miwili, ni pamoja na mikuki iliyotumika kwa ajili ya kujihami na pia mawe ya kombeo kwa ajili ya uwindaji. Korongo la pembeni lina mmomonyoko wa ardhi ulioacha nguzo za ajabu.
Pia vifaa kama nyundo zilizokuwa zikitumika kwa ajili ya kutengenezea zana nyingine na shoka zilizotumika kwa kazi ya kuvunja mifupa, nyembe na visu.
Pia ndani ya eneo hili mafuvu na mifupa mingi vimeonekana; kati yake ilipatikana mifupa ambayo ilifanana na ya twiga wa hivi sasa, ila tofauti ni kwamba, mifupa hiyo iliashiria kuwa twiga hao walikuwa na shingo fupi, ambapo pia kulikuwa na aina tofauti ya viboko.
Remove ads
Picha
- Nguzo za asili, Isimila.
- Mwongozaji wa watalii akiyatazama mawe katika bonde la Isimila
Tazama pia
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads