Kanoaldi

From Wikipedia, the free encyclopedia

Remove ads

Kanoaldi (pia: Chagnoald, Cagnoald, Canoeld, Cagnou, Canoaldus; karne ya 6 - 633 hivi) alikuwa askofu wa 6 wa Laon (Ufaransa) baada ya kuwa mmonaki huko Luxeuil chini ya Kolumbani (594)[1] .

Huyo alipofukuzwa na mfalme Theuderiki II (610), Kanoaldi alikwenda naye kuinjilisha eneo la Bregenz, kando ya ziwa la Konstanz (Ujerumani) [2], halafu aliongozana naye hadi Roma.

Hatimaye aliweza kuongoza jimbo lake hadi alipofariki dunia[3].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu kama ndugu zake Faro na Fara[4].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 6 Septemba[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads