Karne ya 16
karne From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Karne ya 16 ilikuwa kipindi cha miaka mia moja kati ya 1501 hadi 1600. Kikamilifu kilianza tar. 1 Januari 1501 na kuishia 31 Desemba 1600. Namba zake zinafuata hesabu ya miaka "baada ya Kristo".
Kama kila "karne" ni kipindi kinachohesabiwa kwa hiari ya kibinadamu kwa sababu ni mgawanyo wa kalenda tu - hali halisi maendeleo na mabadiiliko makubwa hayafuati migawanyo ya kalenda ya kibinadamu.
Kuna mambo mengi yaliyotokea wakati wa karne hii.
Remove ads
Watu na matukio

- Urekebisho wa Kanisa na Mtaguso wa Trento
- Erasmo wa Rotterdam (Rotterdam 27 Oktoba 1466/1469 - Basel 12 Julai 1536)
- Martin Luther (Eisleben, 1483 - 1546); mwanzo na uenezi wa Uprotestanti
- Vita vya madhehebu Ulaya
- Kalenda ya Gregori
- Koperniki (Torun Polandi, 19 Februari 1473 - Frauenburg, Polandi, 24 Mei 1543), mwanasayansi
- Michelangelo Buonarroti (Caprese, Arezzo, 6 Machi 1475 - Roma, 18 Februari 1564), mwanasanaa bora
- Fransisko Bacone, mwanafalsafa
- Elizabeti I, Malkia wa Uingereza, anaanzisha ukoloni
- William Shakespeare, mwanafasaha bora wa Kiingereza
- Ignas wa Loyola, mwanzilishi wa Wajesuiti
- Teresa wa Yesu na Yohane wa Msalaba wanarekebisha Wakarmeli
Remove ads
Vita
- 1. Vita vya Italia (1494–1559)
Msururu wa migogoro kuhusu udhibiti wa Rasi ya Italia ulioshirikisha Ufaransa, Hispania, Milki ya Kati na mataifa mengine ya Ulaya. Vita hivi vilihusisha miungano iliyobadilika mara kwa mara na mapigano makubwa kote Ulaya.
- 2. Uvamizi wa Japani dhidi ya Korea (1592–1598)
Japani chini ya Toyotomi Hideyoshi ilivamia Korea kwa lengo la kufika Uchina. Korea kwa msaada wa Uchina ya Ming ilizuia uvamizi huo hadi Japani ikajiondoa.
- 3. Vita ya Moroko na Milki ya Songhai (1591)
Moroko ilivamia Milki ya Songhai (katika Mali ya leo), na kuivunja kabisa baada ya ushindi kwenye Vita ya Tondibi.
- 4. Vita vya Miaka Themanini (1568–1648) - 80 years war
Mapambano ya Waholanzi dhidi ya utawala wa Kihispania yaliyosababishwa na mvutano wa kidini na kisiasa. Hatimaye yalipelekea uhuru wa Uholanzi kutoka kwa Himaya ya Hispania.
- 5. Vita kati ya Milki ya Ottoman na Safavid (karne ya 16)
Vita vya mfululizo kati ya Milki ya Kiosmani ya Kisunni na Milki ya Safavid ya Kishia kuhusu udhibiti wa Mesopotamia na maeneo ya Kaukazi ambayo ilichochewa na tofauti za kidini na kisiasa.
- 6. Uvamizi wa Hispania dhidi ya Milki ya Azteki (1519–1521)
Hernán Cortés aliongoza Wahispania kuiangusha Milki ya Azteki katika eneo la leo la Meksiko.
- 7. Vita vya Uingereza na Hispania (1585–1604)
Mapambano kati ya Uingereza ya Kiprotestanti na Hispania ya Kikatoliki, yakiwemo vita vya baharini na mashambulizi ya makoloni. Vilijulikana sana kwa kushindwa kwa Jeshi la Kihispania la Armada.
- 8. Vita vya Livonia (1558–1583)
Vita kati ya Urusi, Polandi-Lithuania, Uswidi na Udeni juu ya udhibiti wa eneo la Bahari ya Baltiki. Urusi ilishindwa na kupoteza maeneo muhimu.
Lango la Historia | Lango la Biografia | Karibuni | Orodha ya Miaka
◄ |
Karne ya 14 |
Karne ya 15 |
Karne ya 16
| Karne ya 17
| Karne ya 18
| ►
Miaka ya 1500 |
Miaka ya 1510 |
Miaka ya 1520 |
Miaka ya 1530 |
Miaka ya 1540 |
Miaka ya 1550 |
Miaka ya 1560 |
Miaka ya 1570 |
Miaka ya 1580 |
Miaka ya 1590
Remove ads
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads