Ludoviko IX

From Wikipedia, the free encyclopedia

Ludoviko IX
Remove ads

Ludoviko IX (maarufu kama Mtakatifu Alois; Poissy, karibu na Paris, Ufaransa, 25 Aprili 1214Tunis, Tunisia, 25 Agosti 1270) alikuwa mfalme wa Ufaransa tangu 1226 hadi kifo chake.

Thumb
Louis IX alivyochorwa na El Greco 15921595 hivi.
Thumb
Sanamu ya Mt. Ludoviko IX huko Paris, Ufaransa.
Thumb
Sanamu yake kama mwanajeshi katika Basilika la Moyo Mtakatifu, Paris.

Anahesabiwa kuwa mtawala bora wa Kikristo kwa jinsi alivyoishi kwa imani wakati wa amani na wakati wa vita alivyovipiga kwa nguvu zote ili kutetea Wakristo waliodhulumiwa, alivyojali ibada, msalaba, taji la miba na kaburi la Bwana, alivyotenda haki katika kuongoza nchi, alivyoheshimu ndoa yake na kulea vizuri watoto wake 11, alivyohudumia wananchi, hasa maskini na wagonjwa, na alivyovumilia matatizo yaliyompata [1].

Alifariki dunia kwa tauni aliyoambukizwa kwa kuwahudumia askari zake wakati wa vita vya msalaba.

Ni mfalme pekee wa nchi hiyo kutangazwa mtakatifu (na Papa Boniface VIII, 1297).

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe aliyoaga dunia[2].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads