Luteni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Luteni (kutoka Kiingereza: Lieutenant), pia Luteni wa Kwanza, ni cheo cha afisa wa jeshi kilicho chini ya Kapteni na juu ya Luteni wa Pili.

Asili ya neno ni Kifaransa "lieu-tenant" (yaani "mwenye kushika nafasi") kwa maana ya naibu, makamu. Kiasili lieu-tenant alikuwa makamu wa kapteni, yaani mkuu wa kikosi aliyeshika mamlaka yake wakati hayuko.
Maana hiyo ni pia asili ya vyeo vya Luteni Kanali au Luteni Jenerali vilivyotaja manaibu wa kanali au jenerali.
Baadaye ziliendelea kuwa vyeo vya pekee bila kuunganishwa na nafasi ya makamu tena.
Majeshi ya Afrika yalirithi cheo hicho sawa na vyeo vya kijeshi kwa jumla kutoka mapokeo ya jeshi la kikoloni.
Makala bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |
Remove ads
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads