Waindio

From Wikipedia, the free encyclopedia

Waindio
Remove ads

Waindio au Wahindi wekundu ni watu wanaotokana moja kwa moja na waliokuwa wenyeji wa Amerika kabla ya bara hilo kufikiwa na Christopher Columbus kutoka Ulaya (1492).

Thumb
Wanawake wa kabila la Quechua katika wilaya ya Andahuaylillas, Peru, 2007.

Asili

Thumb
Ramani ya uenezi wa binadamu duniani[1]

Utafiti uliofanywa kwa muda mrefu na kwa njia mbalimbali umekadiria kwamba mababu wao walioenea katika Amerika yote wakitokea Asia kaskazini mashariki miaka 14,500 BK.

Inadhaniwa kwamba hao mababu waliishi muda mrefu na kuzaliana bila mawasiliano na binadamu wengine, labda katika eneo ambalo leo limefunikwa na maji kwenye mlangobahari wa Bering. Inakadiriwa DNA yao ilitokana na ile ya Waasia mashariki (2/3) na Waeurasia (1/3).

Baada ya kuingia bara hilo, ambalo ni la mwisho kukaliwa na watu (tukiacha Antaktiki), kwa karne chache walienea hadi kusini kabisa, kwenye Chile na Argentina ya leo. Katika kusambaa kwao, lugha na utamaduni vilizidi kutofautiana.

Remove ads

Hali ya sasa

Idadi yao inaweza kuwa milioni 60, wengi wao wakiishi Meksiko, Peru, Bolivia na Guatemala.

Hesabu hii haijumlishi machotara.

Tanbihi

Vyanzo

Loading content...

Marejeo

Loading content...

Marejeo mengine

Viungo vya nje

Loading content...
Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads