Maria Magdalena Postel
From Wikipedia, the free encyclopedia
Remove ads
Maria Magdalena Postel, ambaye jina la kiraia kwa Kifaransa lilikuwa Julie Françoise-Catherine Postel (Barfleur, Ufaransa, 28 Novemba 1756 - Saint-Sauveur-le-Vicomte, 16 Julai 1846) alikuwa mwanamke ambaye mwaka 1807 alianzisha shirika la Masista wa Shule za Kikristo wa Huruma (Congrégation des sœurs des Écoles chrétiennes de la Miséricorde) kwa ajili ya malezi ya Kikristo ya wasichana fukara [1].

Alitangazwa na Papa Pius X kuwa mwenye heri mwaka 1908 akatangazwa na Papa Pius XI kuwa mtakatifu tarehe 24 Mei 1925.
Remove ads
Maisha
Mwaka 1774 huko Barfleur Julie Postel alifungua shule ya wasichana ambayo wakati wa mapinduzi ya Ufaransa ilitumika kwa shughuli za kidini za siri za Wakatoliki waliokataa masharti ya serikali yaliyo.
Baada ya dhuluma kwisha, aliendelea kufundisha na kufanya kazi nyingine za huruma.
Alipofikia umri wa miaka 51 aliweka nadhiri kwa jina la sista Maria Magdalena akaandaa uanzishaji wa shirika.
Miaka ya kwanza mafanikio yalikuwa madogo, lakini mwaka 1830 alifaulu kununua monasteri ya zamani huko St-Sauveur-le-Vicomte iwe makao makuu.
Shirika lilikubalika rasmi mwaka 1837 likabaki chini ya usimamizi wa mwanzilishi hadi mwaka wake wa mwisho.[3]
Remove ads
Tazama pia
Tanbihi
Marejeo
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Remove ads