Monika

From Wikipedia, the free encyclopedia

Monika
Remove ads

Monika (Tagaste, Numidia, leo Algeria 332 - Ostia, kitongoji cha Roma, Italia, 387) alikuwa mwanamke wa kabila la Kiafrika la Waberberi ambaye aliolewa mapema na Patricius, afisa wa Dola la Roma, akamzalia watoto, mmojawao Agostino wa Hippo[1].

Thumb
Monika na mwanae Augustino.

Kwa ajili ya uongofu wake alisali sana na kutoa machozi mengi mbele ya Mungu hadi akasikilizwa. Ndipo alipopotewa na hamu ya kuishi akatamani tu kwenda mbinguni akafariki dunia kabla hajarudi Afrika [2].

Ni maarufu hasa kutokana na sifa alizomwagiwa mwanae huyo katika kitabu cha Maungamo (Confessiones).

Anaheshimiwa na madhehebu mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu, hasa tarehe 27 Agosti[3] au 4 Mei.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Marejeo ya Kiswahili

Marejeo ya lugha nyingine

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads