Nabii Shemaya

From Wikipedia, the free encyclopedia

Nabii Shemaya
Remove ads

Nabii Shemaya (kwa Kiebrania שְׁמַעְיָה, Šəmaʿyā, maana yake: "YHWH amesikia"; alikuwa nabii nchini Israeli katika karne ya 10 KK.

Thumb
Picha takatifu ya Kiorthodoksi ya Ugiriki ya Nabii Shemaya.
Thumb
Sanamu ya Shemaia katika Chuo Kikuu cha Liverpool.

Chanzo kikuu cha historia yake ni Kitabu cha Kwanza cha Wafalme (12:22-24) pamoja na Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati (11:2-4; 12:5-7).

Kadiri ya vitabu hivyo, alimzuia mfalme Rehoboamu asipigane vita na Yeroboamu I ili kujirudishia mamlaka juu ya makabila ya kaskazini yaliyoasi[1].

Pia alimtabiria Rehoboamu adhabu ya Mungu kumpitia farao Shishak wa Misri kwa makosa yake.

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Januari.

Remove ads

Mengineyo

Katika Biblia ya Kiebrania kuna watu wengine kumi na saba wenye jina hilohilo, tena inataja Kitabu cha nabii Shemaya kama chanzo cha habari kadhaa, lakini kitabu hicho kimepotea hata leo.

Tazama pia

Tanbihi

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads