Papa Agatho

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Agatho
Remove ads

Papa Agatho alikuwa Papa kuanzia tarehe 27 Juni 678 hadi kifo chake tarehe 10 Januari 681[1]. Alitokea Sicilia, Italia[2][3].

Thumb
Papa Agatho.

Alitetea imani sahihi dhidi ya wazushi waliosema Yesu hakuwa na utashi wa kibinadamu na aliendesha sinodi kadhaa ili kuimarisha umoja wa Kanisa.

Inasemekana kwamba alikuwa na umri wa zaidi ya miaka mia moja alipochaguliwa kuwa Papa, na alikuwa ametunza hazina ya Kanisa kwa miaka mingi[4].

Wakati wa Upapa wake ulifanyika Mtaguso wa tatu wa Konstantinopoli (680-681) uliofundisha rasmi kwamba Yesu, chini ya utashi wake wa Kimungu, alikuwa na utashi wa kibinadamu pia[5].

Alimfuata Papa Donus akafuatwa na Papa Leo II.

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Kanisa Katoliki linaadhimisha sikukuu yake tarehe 10 Januari[6], lakini Waorthodoksi tarehe 20 Februari.

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads