Papa Dionysius

From Wikipedia, the free encyclopedia

Papa Dionysius
Remove ads

Papa Dionysius alikuwa Papa kuanzia tarehe 22 Julai 259 hadi kifo chake tarehe 26 Desemba 269[1].

Thumb
Papa Dionysius.

Alimfuata Papa Sisto II akafuatwa na Papa Felisi I.

Alifanya kazi kubwa ya kupanga upya Kanisa baada ya dhuluma ya kaizari Valerian iliyoacha Roma bila askofu kwa karibu mwaka mzima[2]. Mtu aliyejaa maadili mema, alitumia uhuru uliopatikana upya chini ya kaisari Gallienus na kudumu miaka 40 [3], akifariji kwa barua zake na uwepo wake ndugu wenye huzuni, akikomboa wafungwa katika mateso yao na kuwafundisha misingi ya imani wasioijua [4].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 26 Desemba[5].

Remove ads

Tazama pia

Tanbihi

Maandishi yake

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Remove ads